From Wikipedia, the free encyclopedia
Kakakuona (kwa Kiingereza: pangolin) ni wanyama wa familia Manidae ambao wamepambika na magamba na wana mkia mrefu. Wakitaka kujikinga dhidi ya wanyama mbuai wanajikunja.
Kakakuona | ||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kakakuona-nyika | ||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||
| ||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||
Jenasi 3, spishi 8:
| ||||||||||
Huishi katika shimo la kina cha hadi mita 3.5 au katika mti mvungu.
Hula mchwa na sisimizi na pengine wadudu wengine ambao huwakamata kwa ulimi wao mrefu wenye kunata.
Kakakuona-nyika anapatikana Hifadhi ya Serengeti.
Huzaa kidogo sana, na hiyo imechangia kufanya wapungue sana. Sababu nyingine ni ushirikina unaodai wanaleta bahati njema, hasa magamba yao. Ndiyo sababu nchini Tanzania wanalindwa na sheria kali hata wasikamatwe.
Hata hivyo, kakakuona wanawindwa sana wakiwa katika hatari ya kupotea. Kwenye Desemba 2019 magazeti yalitoa taarifa kuwa uwindaji haramu wa kakakuona unaongezeka hasa kwa sababu wanatafutwa kwenye masoko ya Asia. Katika nchi kama China na Vietnam nyama yao hutazamwa chakula kitamu, magamba yao hutumiwa katika dawa za jadi na ngozi hutumiwa kwa viatu au nguo. Tangu kupigwa marufuku kwa biashara ya spishi za kakakuona za Asia, biashara inalenga spishi za Afrika. Mwaka 2019 tani 6 za magamba ya kakakuona zilikamatwa na maafisa wa wizara ya maliasili katika Mkoa wa Morogoro.[1]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.