From Wikipedia, the free encyclopedia
Idd el Hajj (pia: Idi el haji, eid el hajj) ni sikukuu ya Uislamu wakati wa mwezi wa Dhul Hijjah ambao ni mwezi wa Hajj. Sherehe hii inatunza kumbukumbu ya sadaka ya Ibrahimu.
Kati ya Waislamu duniani sikukuu hii hujulikana kwa majina mbalimbali ambayo hutafsiriwa pia kwa lugha mbalimbali kama vile:
Idd husheherekewa kama kumbukumbu ya sadaka ya Ibrahimu (Abrahamu) ambaye kufuatana na taarifa za Biblia na za Qurani alikuwa tayari kumchinja mwanawe kama sadaka kwa Mungu. Lakini Mungu alimzuia asimchinje akampatia kondoo badala yake. Habari zake kati Qurani ziko sura al-Hajj aya 37, katika Biblia Mwanzo 22.
Katika mapokeo ya Biblia huyu mwana alikuwa Isaka. Qurani haitaji jina lake lakini Waislamu walio wengi huamini aliyemaanishwa ni Ismaeli, mwana wa Ibrahimu na Hagar.
Sherehe huanza na sala ya idd katika msikiti. Mara nyingi hufuatwa na baraza au mkutano wa Waislamu. Katika nchi nyingi huwa na kawaida ya kutembelea pia makaburi ya marehemu.
Kila Mwislamu mwenye uwezo hupaswa kumchinja mnyama wa sadaka siku hiyo, mara nyingi kondoo, lakini kuna pia sadaka za mbuzi, ng'ombe au ngamia kufuatana na uwezo na kawaida ya nchi.
Sehemu ya nyama ya sadaka hizo hugawiwa kwa maskini wasio na uwezo. Nyingine hutumiwa kwa karamu ya familia.
Idd husheherekewa kati ya tarehe 10 hadi 13 ya mwezi wa Dhul Hijjah wa kalenda ya Kiislamu. Tarehe hali halisi hutegemea kuonekana kwa hilali au mwezi mwandamo. Hapa hutokea tofauti za kila mwaka kati ya Waislamu. Kimsingi mapokeo ya Kiislamu hudai mwezi kuonekana kwa macho.
Sehemu za Waislamu hukubali ya kwamba inawezekana kukadiria tarehe hii kisayansi, lakini huko Saudia husisitizwa kuona kwa macho. Maadamu Saudia ni mahali pa miji mitakatifu ya Maka na [Madina]], Waislamu wengine hupenda kufuata kawaida ya kule.
Zamani hapakuwa na tatizo sana kwa sababu kila nchi ilikuwa na azimio lake. Mitambo ya kisasa huonyesha siku hizi kama Waislamu wameshaanza kusheherekea nchi moja lakini nchi nyingine bado. Katika nchi mbalimbali, hasa kule ambako Waislamu walihamia juzi tu kama Ulaya, kuna tarehe tofauti kandokando kama wengine hufuata matangazo ya Uturuki yanayokadiriwa kisayansi na wengine matangazo ya Saudia yanayofuata kuonekana kwa macho. Matangazo ya Saudia yamepingwa mara nyingi kwa sababu tarehe zilitangazwa ambapo hapakuwa na uwezekano kuona hilali kisayansi.
Katika kalenda ya Gregori, ambayo ni kalenda ya kawaida, tarehe za Kiislamu hubadilika kila mara kwa sababu mwaka wa Kiislamu hufuata kalenda ya mwezi lakini kalenda ya kawaida hufuata jua. Kalenda ya Kiislamu ina takriban siku 11 pungufu kuliko kalenda ya jua. Kila mwaka tarehe ya Idd huweza kutokea kwa siku mbili tofauti za kalenda ya Gregori kwa sababu kawaida ya Uislamu hufuata kuonekana kwa mwezi kunakopatikana tofauti duniani.
Orodha inyaofuata yaonyesha tarehe rasmi za Idd-al-Hajj kwa nchi ya Saudia jinsi ilivyotangazwa hadi 2007 na halmashauri kuu ya Majlis al-Qadā’ al-A‘lā . Tarehe za miaka 2008 na kuendelea ni tarehe zinazokadiriwa kulingana na kalenda ya Kiislamu jinsi ilivyo kawaida katika nchi kama Uturuki. Tofauti zitaendelea kutokea kulingana na maelezo hapo juu kuhusu tofauti ya makadirio na kuonekana kwa hilali
Makala hii kuhusu Uislamu bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.