From Wikipedia, the free encyclopedia
Horus alikuwa mmoja wa miungu ya Misri ya Kale. Katika mitholojia ya Kimisri alikuwa mwana wa Isis na Osiris. Aliabudiwa hasa kama mungu wa anga na pia mungu wa ufalme.
Ibada yake iliendelea kwa muda mrefu, kuanzia nasaba ya kwanza hadi wakati wa Misri ya Kiroma. Katika kipindi hicho mawazo mengi kuhusu Horus yalitokea akaabudiwa kwa maumbo mengi tofauti.
Lakini umbo kuu lilikuwa ndege ya kozi au mwanadamu mwenye kichwa cha kozi.
Horus, aliabudiwa kote Misri, haswa huko Pe, Bendet na Khem .
Horus alichukuliwa kuwa mzuri na kawaida alionekana kama kozi au mtu mwenye kichwa cha kozi, ingawa wakati mwingine alionekana kama mamba mwenye kichwa cha kozi. Kwa kawaida alivaa taji maradufu kuashiria utawala wake juu ya Misri yote na uhusiano wake kama mlinzi wa Farao.
Horus alikuwa mungu wa anga na pia mungu wa vita. Kila farao wa Misri alitazamwa na kuheshimiwa kama Horus aliye hai. Alipofariki, farao aliendelea kutazamwa kama Osiris, mungu wa wafu na baba wa Horus. Farao mpya alikuwa Horus. Aliaminiwa anamlinda farao. Alikuwa mungu mlinzi, ambaye alikuwa mungu aliyepigana na uovu. Aliwakilisha haki.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.