Helena (kwa Kigiriki: Ἑλένη, Helénē; kwa Kilatini: Flavia Iulia Helena Augusta; 246/248 – Roma, 330 hivi) alikuwa mke wa kaisari Constantius Chlorus.

Thumb
Sanamu ya Mt. Helena, Musei Capitolini, Roma, Italia.

Alijitokeza kwa bidii zake za kusaidia fukara; pia alikuwa anaingia makanisani kwa moyo wa ibada akijichanganya na umati wa waumini [1].

Alipohiji Yerusalemu ili kuheshimu mahali pa kuzaliwa, kuteseka na kufufuka Yesu Kristo, alitembelea pango na msalaba wake akapajengea mabasilika ya fahari [2].

Ni maarufu hasa kama mama wa Konstantino Mkuu aliyemuelekeza kupenda Ukristo na hivyo alichangia uanzishaji wa uhuru wa dini katika Dola la Roma baada ya miaka 250 ya dhuluma dhidi yake.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 18 Agosti[3] au 21 Mei.

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.