Mlangobahari wa Denmark (kwa Kiingereza: Denmark Strait au Greenland Strait; kwa Kidenmark: Danmarksstrædet; kwa Kiiceland: Grænlandssund) ni sehemu ya Bahari Atlantiki inayotenganisha Greenland upande wa kaskazini na Iceland upande wa kusini. Kisiwa cha Jan Mayen cha Norwei kiko upande wa mashariki wa mlangobahari huo.

Thumb
Ramani ya Bahari ya Norwei.
Thumb
Mapande ya barafu katika Mlangobahari wa Denmark.

Mlangobahari wa Denmark unaunganisha Bahari ya Greenland (sehemu ya Bahari Aktiki) na Bahari Atlantiki. Una urefu wa kilomita 480 na upana wa km 290.

Upande wa magharibi wa mlangobahari huo kuna maporomoko makubwa chini ya uso wa bahari ambako maji baridi kutoka Aktiki hushuka zaidi ya mita 3,000 kuelekea vilindi vya Atlantiki. Maporomoko hayo ni sehemu muhimu ya mzunguko wa maji wa Atlantiki.

Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia, tarehe 24 Mei 1941, yalitokea mapigano ya baharini baina ya manowari kubwa "Bismarck" ya Ujerumani na manowari za Uingereza.


67°N 24°W

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.