From Wikipedia, the free encyclopedia
Gundi (kutoka Kiingereza: gundi) au panya-kichanuo (kutoka Kiingereza: comb rat) ni wagugunaji wadogo wa familia Ctenodactylidae wanaotokea kaskazini kwa Afrika. Huishi katika majangwa yenye miwamba. Mwili wao ni mnono wenye urefu wa sm 17-18 na unafunikwa kwa manyoya laini. Wana miguu mifupi, macho makubwa na mkia mfupi. Miguu yote ina vidole vinne tu na vile vya kati vya miguu ya nyuma vina nywele ngumu zinazofananana na kichanuo (sababu ya jina la panya-kichanuo). Hula kila aina ya mmea ipatikanayo, lakini, kama wanyama wengi wa jangwa, hawakunywi na hupata maji yote wanayoyahitaji kutoka chakula chao[1]. Jike huzaa watoto wawili kila mara baada muda wa mimba wa mieze miwili. Kwa sababu ya uhitaji wa kuhifadhi maji jike hutoa maziwa machache tu na watoto hulikizwa kabisa baada ya wiki nne.
Gundi | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Gundi kaskazi (Ctenodactylus gundi) | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Jenasi 4, spishi 5:
| ||||||||||||
Gundi huishi katika makoloni ya wanyama hadi mia moja au zaidi, lakini idadi ni ndogo katika maeneo ambapo chakula ni adimu. Hawatengenezi matundu ya aushi lakini hujisitiri katika mianya ya miamba usiku au mchana wakati wa joto kubwa. Wanyama hawa hufanya sauti sana na wana namba ya sauti za alamu na mawasiliano ambazo zinawasaidia kwa kugundisha makundi yao.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.