From Wikipedia, the free encyclopedia
Korobindo ni ndege wadogo wa jenasi mbalimbali katika familia Passeridae. Kuna ndege wengine ambao wanaitwa korobindo katika familia Ploceidae. Spishi za ukurasa huu zinatokea Afrika isipokuwa (Chestnut-shouldered Petronia) ambaye anatokea Asia. Korobindo-mawe anatokea Ulaya pia na korobindo-msitu na korobindo hudhurungi Asia pia. Ndege hawa wanafanana na shomoro, lakini rangi yao ni vivu zaidi. Madume wa jenasi Gymnoris wana doa njano chini ya koo ambalo ni ngumu kuona kwa kawaida. Hula mbegu, beri, mbochi na wadudu. Wanalijenga tago lao kwa nyasi na manyoya katika tundu mtini au pengine ukutani. Jike huyataga mayai 3-5.
Korobindo | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Korobindo koo-njano | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Jenasi 3, spishi 6:
| ||||||||||||
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.