From Wikipedia, the free encyclopedia
Ngamia ni wanyama wakubwa wa jenasi Camelus katika familia Camelidae inayowajumlisha pamoja na lama na vikunya wa Amerika Kusini.
Ngamia | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Ngamia nundu-moja (Camelus dromedarius) | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Spishi 2:
| ||||||||||||||
Spishi zote mbili wamezoea kuishi katika mazingira yabisi kama jangwa au nusu jangwa.
Ngamia nundu-moja anapatikana katika Uarabuni, Mashariki ya Kati hadi Pakistani, Afrika ya Kaskazini, Somalia na kaskazini ya Kenya. Katika karne ya 19 walipelekwa Australia walipozoea haraka; kwa sasa takribani ngamia pori 700,000 wako kule. Spishi hii inavumilia joto kali lakini pia baridi za usiku kwenye Sahara. Anaweza kubadilisha halijoto ya mwili wake kati ya sentigredi 34 na 41 kulingana na mazingira.
Ngamia wa Asia yuko katika kanda inayoanzia Anatolia hadi Manchuria kaskazini mwa China. Amezoea zaidi baridi ya Asia ya Kati; wakati wa majira barafu halijoto ya mazingira inafikia -30°C. Joto kali inampa matatizo kidogo na kumchelewesha.
Spishi zote mbili zinakutana katika nchi kadhaa, kuanzia Uturuki, Uajemi, Afghanistan hadi Pakistani.
Umbile lao limelingana na mazingira ya jangwani. Miguu ni mipana na kuzuia wasizame chini kwenye mchanga. Nywele ni ndefu, hivyo zinakinga dhidi ya joto na baridi.
Nundu ni mahali pa stoo ya akiba ya mafuta; kama ngamia anapitia mahali pasipo chakula anatumia mafuta kwa nishati ya mwilini. Hahitaji kula kwa kipindi hadi siku 30.
Wanaweza kushika lita 100–150 mwilini na kuendelea jangwani bila kunywa maji kwa wiki mbili. Penye majani mabichi ya kutosha, na kama joto si kali mno, ngamia anaweza kuendelea bila kunywa kwa wiki kadhaa.
Shingo ni ndefu kwa sababu kwa chakula anapendelea majani ya miti na vichaka.
Ngamia ni wanyama wa kijamii na kwa asili huishi katika makundi ya dume mmoja na majike kadhaa. Siku hizi kuna ngamia wa Asia mamia kadhaa kwenye pori ambao ni mabaki ya ngamia pori wa zamani. Wako China na Mongolia.
Ngamia nundu-moja si wanyama wa pori asilia tena; inaaminiwa walitokea Uarabuni. Lakini kuna wanyama waliotoroka huko Australia na Amerika wanaoishi peke yao, hawafugwi.
Ngamia wamefugwa na binadamu tangu miaka 5,000–6,000 iliyopita. Leo hii mifugo hao ni takriban milioni 19 na idadi kubwa, yaani milioni 14, wako Afrika, milioni 7 pekee nchini Somalia na milioni 3.3 nchini Sudan.
Watu hufuga ngamia kwa kubeba watu na mizigo. Nywele zao ni aina ya sufu inayotumiwa kutengenezea mashuka, mahema na pia vitambaa vya nguo. Wanachinjwa kwa nyama yao.
Ngamia hukamuliwa pia kama ng'ombe. Katika nchi yabisi kiasi cha maziwa yao yanalingana na ya ng'ombe.
Katika miaka ya nyuma Wamasai wa Kenya na pia Tanzania wameanza kufuga ngamia baada ya kuona ya kwamba ng'ombe zao walikufa wakati wa ukame lakini ngamia waliendelea kuishi na kutoa maziwa.
Ngamia anachukua chakula chake kwenye mti wenye mizizi mirefu kushinda manyasi yanayoliwa na ng'ombe. Kwa sababu hiyo manyasi hukauka haraka wakati wa ukame kuliko majani ya miti.
Katika mazingira ambako Biblia iliandikwa, ngamia alikuwa mnyama mkubwa kuliko wote wa nchi kavu. Ndiyo sababu alitumika katika methali mbalimbali kwa kusisitiza jambo.
Kwa mfano, Yesu alisema, "Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu la sindano kuliko tajiri kuingia mbinguni" (Mk 10:23-27).
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.