From Wikipedia, the free encyclopedia
Bahari ya Ross ni sehemu ya Bahari ya Kusini iliyopo katika hori kubwa huko Antaktiki kati ya Nchi ya Viktoria na Nchi ya Marie Byrd.
Bahari ya Ross iligunduliwa na nahodha Mwingereza James Ross mnamo 1841. Magharibi mwa Bahari ya Ross kipo Kisiwa cha Ross. Mashariki kiko Kisiwa cha Roosevelt. Sehemu ya kusini imefunikwa na barafu. [1] Katika magharibi mwa bahari ya Ross kuna bandari ambayo kwa kawaida huwa haina barafu wakati wa kiangazi.
New Zealand inadai usimamizi juu ya maeneo yote katika Bahari ya Ross.
Katika msimu wa joto kuna planktoni nyingi ambayo ni muhimu kama chanzo cha chakula kwa spishi kubwa kama vile samaki, sili, nyangumi, na ndege wa bahari.
Kwenye pwani za bahari hii kuna sehemu ambapo spishi mbalimbali za ngwini hukutana na kuzaa. [1]
Bahari ya Ross ni mojawapo ya sehemu za mwisho za bahari duniani zisizoathiriwa bado na shughuli za wanadamu. Kwa sababu hiyo hakuna uchafuzi wa mazingira.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.