From Wikipedia, the free encyclopedia
Angatando (pia angastrato; Kiingereza: stratosphere) ni tabaka mojawapo la angahewa ya Dunia[1]. Inaanza takriban kilomita 8 juu ya uso wa ardhi kwenye eneo la ncha za Dunia lakini juu ya ikweta inaanza kwa kimo cha kilomita 18; inaendelea hadi kimo cha kilomita 50 juu ya uso wa ardhi[2].
Katika angastrato, kiunyume na angatropo, halijoto inapanda juu pamoja na kimo. Hii inasababishwa na tabaka la ozoni iliyoko ndani yake. Ozoni hufyonza mnururisho wa urujuanimno kutoka nuru ya Jua na kuibadilisha kuwa joto[3].
Hii ni tofauti na angavurugu iliyoko chini yake. Huko halijoto inapungua kadiri ya kuongezeka kwa kimo. Pia katika angakati iliyoko juu ya tabakastrato halijoto inapungua kadiri ya kufikia juu zaidi.
Hakuna upepo wala mawingu katika angastrato, hivyo eropleni kubwa husafiri pale inapoanza kwenye kimo cha km 12 kwa safari za mbali ambako vurugu kutokana na upepo wa angavurugu zimeshapungua [4].
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.