![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/2/28/Tanzania_Arumeru_location_map.svg/langsw-640px-Tanzania_Arumeru_location_map.svg.png&w=640&q=50)
Wilaya ya Meru
Wilaya iliomo Mkoa wa Arusha. / From Wikipedia, the free encyclopedia
Wilaya ya Meru ni wilaya mojawapo ya Mkoa wa Arusha yenye postikodi namba 23300.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/2/28/Tanzania_Arumeru_location_map.svg/250px-Tanzania_Arumeru_location_map.svg.png)
Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa Wilaya ya Meru ilihesabiwa kuwa 268,144 [1]. Katika ile ya mwaka 2022 walihesabiwa 331,603 [2].
Wilaya hiyo ilianzishwa kutoka maeneo ya wilaya ya zamani ya Arumeru iliyogawiwa kuwa wilaya ya Arusha Vijijini na wilaya ya Meru.
Makao makuu ya wilaya yako mjini Usa River.