Wilaya ya Gucha
From Wikipedia, the free encyclopedia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Wilaya ya Gucha (pia: Wilaya ya Kisii Kusini au Wilaya ya Ogembo) ilikuwa wilaya mojawapo ya Mkoa wa Nyanza wa Jamhuri ya Kenya hadi ilipopitishwa katiba ya katiba mpya ya nchi (2010). Jina limetokana na mto Gucha
Makao makuu yalikuwa Ogembo, yenye wakazi zaidi ya elfu moja na wageni zaidi ya elfu moja ambao huitembelea kila siku.
Kwa sasa imekuwa kaunti ndogo ya kaunti ya Kisii ikiwa na South Bogirango Gucha North Bogirango.
Wakazi wake walikuwa takriban 461,000 (1999) [1]. Idadi kubwa ya watu ni Wakisii, lakini hupakana na ardhi ya Wamasai huko kusini-mashariki. Kumekuwa na mapigano kadhaa ya kikabila baina yao.
Kilimo ndiyo sekta kuu. Mbali ya mashamba mengi madogo madogo, kuna mashamba makubwa ya miwa.
Wilaya hii ilikuwa na majimbo matatu: South Mugirango, Bomachoge na Bobasi. Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2002 viti vyote vitatu vilishindwa na chama cha Ford-People.
Mamlaka za Mitaa (Halmashauri) | |||
Mamlaka | Aina | Idadi ya Watu | Wakazi wa mjini* |
---|---|---|---|
Ogembo | Jiji | 48.725 | 1.654 |
Nyamarambe | Jiji | 40.232 | 212 |
Nyamache | Jiji | 38.924 | 2.205 |
Tabaka | Jiji | 26.325 | 5.067 |
Gucha | County | 306.733 | 1.946 |
Jumla | -- | 460.939 | 11.084 |
* 1999 census. Source: |
Maeneo ya utawala | |||
Tarafa | Idadi ya Watu | Wakazi wa mjini* | Makao makuu |
---|---|---|---|
Etago | 59.652 | 0 | |
Kenyenya | 92.641 | 1.857 | |
Nyacheki | 56.998 | 405 | |
Nyamache | 54.722 | 1.702 | |
Nyamarambe | 67.060 | 3.850 | |
Ogembo | 78.827 | 1.465 | Ogembo |
Sameta | 51.039 | 0 | |
Jumla | 460.939 | 9.279 | -- |
* 1999 census. Sources: , , |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.