Watitani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Watitani (kutoka Kigiriki: Τiτᾶνες , titânes - "wanaojikazia") walikuwa nasaba ya pili ya miungu katika mitholojia ya Kigiriki. Jina hilo linataja idadi ya miungu 12 ambao, katika masimulizi ya Wagiriki wa Kale, walikuwa watoto wa Gaia na Uranos.
Katika imani ya Wagiriki wa Kale walitawala ulimwengu kabla ya nasaba ya miungu wa Olimpos, ambao walipigania udhibiti wa ulimwengu katika mfululizo wa vita kadhaa unaojulikana kama vita ya Watitani (titanomachy). Waolimpo walishinda na Waitani wengi walifukuzwa mbinguni na kufungwa katika vilindi vya Tartaro.