Vita vya Ufaransa na Waindio
From Wikipedia, the free encyclopedia
Vita vya Ufaransa na Waindio vilikuwa vita vya kimataifa kutoka mwaka wa 1754 hadi mwaka wa 1763. Vita vilitokea baada ya miaka mingi ya mapigano kati ya Uingereza, Hispania, na Ufaransa katika maeneo ya kikoloni ya Amerika Kaskazini. Waindio waliingia vitani pande zote mbili, kadiri ya makabila yao.
Vita hivyo vinatazamwa kwa kawaida kama sehemu ya Vita vya Miaka Saba vilivyoenea katika kontinenti tano miaka 1756-1763.