![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/14/Giotto_-_Legend_of_St_Francis_-_-05-_-_Renunciation_of_Wordly_Goods.jpg/640px-Giotto_-_Legend_of_St_Francis_-_-05-_-_Renunciation_of_Wordly_Goods.jpg&w=640&q=50)
Ufukara wa hiari
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ufukara wa hiari ni hali ya maisha ambayo baadhi ya watu wanaichagua kwa sababu za kifalsafa, za kimaadili na hasa za kidini. Katika Ukristo ni maarufu hasa Antoni abati na Fransisko wa Asizi.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/14/Giotto_-_Legend_of_St_Francis_-_-05-_-_Renunciation_of_Wordly_Goods.jpg/640px-Giotto_-_Legend_of_St_Francis_-_-05-_-_Renunciation_of_Wordly_Goods.jpg)
Thamani ya ufukara huo inaeleweka kwa kuzingatia fujo zinazotokana na tamaa ya vitu, uchu wa mali, choyo, ubepari na usahaulifu wa njaa inayoua mafukara. “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha” (1Tim 6:10). “Kinyume cha mema ya Kiroho, malimwengu yanatenganisha watu, kwa kuwa hayawezi kuwa ya wengi kwa mkupuo moja na kikamilifu” (Augustino). Hivyo utafutaji wake usiporatibiwa unatenganisha, wakati utafutaji wa mema ya Kiroho unaunganisha watu. Kwa mfano, Mungu tunaye kadiri tunavyomshirikisha kwa wenzetu, kumbe tukiwanyima tunakuja kumkosa.