Ufalme wa Merina
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ufalme wa Merina ni mlolongo wa watu ambao waliwahi kuwa watawala wa Bukini (sasa inafahamika zaidi kama Madagaska) katika kipindi cha miaka themanini kuanzia mwaka 1787 hadi mwaka 1897.
Watawala hao walikuwa watu kutoka familia ya Andrianampoinimerina, mwanzilishi wa taifa hilo ambaye alikuwa ametokea katika kabila la Wamerina ambalo ndilo lilikuwa kabila lilioenea sehemu kubwa ya Bukini.
Watawala hao wa kifalme waliweza kutekeleza mambo mbalimbali kuendeleza Bukini katika vipindi vyao kabla ya kuja kwa utawala wa kigeni wa Uingereza na Ufaransa ambao kwa kiasi fulani ulidhoofisha mamlaka ya kifalme.