Kenda
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kenda ni Kiswahili asilia kwa namba 9. Kwa kawaida inaandikwa 9 lakini IX kwa namba za Kiroma na ٩ kwa zile za Kiarabu.
Vigawo vyake vya namba tasa ni: 3 x 3.
Neno hili ni la asili ya Kibantu. Siku hizi neno "tisa" ambalo ni neno lenye asili ya Kiarabu hutumiwa zaidi kutaja namba 9, pamoja na tisini (tisa mara kumi).
Kamusi za mwanzo na katikati ya karne ya 20 kama M-J SSE zinasema ya kwamba "kenda" iliwahi kutumiwa sawa na "tisa".
Siku hizi matumizi yake imepungua sana.
Mfano wa matumizi yake ni katika jina Mijikenda linalotaja kundi la makabila au koo 9 za Kenya.