Surat
From Wikipedia, the free encyclopedia
Surat ni mji wa Jimbo la Gujarat nchini Uhindi. Uko kwenye kingo za mto Tapti, karibu na mdomo wake katika Bahari Hindi. Hivyo ilikuwa bandari muhimu lakini siku hizi maji yake hayana kina cha kutosha kwa meli kubwa. Ni jiji lenye wakazi milioni 4.5 lenyewe, na milioni 6 katika rundiko la mji. Ni mji mkubwa wa nane nchini Uhindi.
Ukweli wa haraka
Nchi | Uhindi |
Jimbo / Mkoa | Gujarat |
Anwani ya kijiografia | 21°10′12.864″N 72°49′51.819″E |
Kimo | mita 13 |
Eneo | km2 326.515 [1] |
Wakazi | 4,467,797[2] |
Msongamano wa watu | 14,000/km2 |
Simu | 91-261-XXX-XXXX |
Tovuti rasmi | www.suratmunicipal.gov.in |
Funga