Sululu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Sululu ni ndege wa jenasi mbalimbali katika familia ya Scolopacidae. Hata jenasi Numenius huitwa sululu, lakini jina membe linastahabiwa. Ndege hawa wana rangi zilizofifia na hawaonekani rahisi wotoni. Huruka tu wakati mtu anapowakaribia sana. Wana miguu mifupi na mdomo mrefu. Wapenda mahali majimaji na hula wadudu na nyungunyungu. Wakati wa majira ya kuzaa dume hufanya mkogo wa kubembeleza jike akishuka ghafla angani na kusabibisha manyoya maalum ya mkia kutoa uvumi kubwa. Hujenga tago kwa manyasi linalofichwa sana na jike huyataga mayai 3-4.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...
Sululu | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Sululu wa Ulaya | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Funga