Elimu ya sekondari
From Wikipedia, the free encyclopedia
Elimu ya sekondari (shule za upili), katika mifumo ya kisasa ya elimu ulimwenguni, huchukua kipindi cha pili cha elimu rasmi ambayo hutokea wakati wa ujana wa wanafunzi.
Mfumo huu hutofautiana na masomo ya msingi ambayo ni ya lazima, ni ya jumla na yanayofanana. Yale ya shule za upili ni teule na ya hiari. Shule hizi hujulikana kama sekondari, shule za upili, shule za kati, vyuo au shule za ujuzi wa kitaalamu kulingana na kipindi au mfumo unaofuatwa.
Maana ya dhana hizi hutofautiana kutoka mfumo mmoja hadi mwingine. Mpaka kamili kati ya elimu ya msingi na ya upili hutofautiana kutoka nchi moja hadi nyingine. Tofauti hizi zipo hata katika nchi, lakini kwa jumla hutokea kati ya mwaka wa saba na wa kumi wa kusoma.
Elimu ya sekondari hutokea katika umri wa ujana. Nchini Marekani na Kanada, elimu ya msingi na sekondari kwa pamoja hurejelewa kama elimu ya K-12 na nchini Nyuzilandi, elimu hii hurejelewa kama elimu ya miaka 1-13. Azma ya elimu ya sekondari ni kutoa maarifa ya kawaida, kutayarisha wanafunzi kwa elimu ya juu au kuwafunza kazi moja kwa moja.
Tunapaswa kujitahidi katika kuhamasisha elimu ya sekondari kwani huwezesha kufikia chuo kikuu.