Bundi (pia mabundi) ni ndege mbuai wa familia Tytonidae na jenasi mbalimbali ya familia Strigidae. Ukurasa huu unahusu familia Tytonidae. Spishi hizi zina rangi ya kahawa nyuma na nyeupe mbele pamoja na madoa madogo meusi. Kichwa chao kina umbo la mviringo na uso mwao una umbo la moyo. Bundi hula ndege na wanyama wadogo, wanyama wagugunaji hasa, lakini wadudu wakubwa pia. Jike huyataga mayai 2-7 kwa mahali palipofunika kama tago lililoachwa na ndege mwingine ndani ya tundu ya mti, ufa wa mwamba, dari la nyumba au kihenge n.k.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...
Bundi
Thumb
Bundi-mbuga
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Strigiformes (Ndege kama bundi)
Familia: Tytonidae (Ndege walio na mnasaba na bundi)
Jenasi: Phodilus I. Geoffroy Saint-Hilaire, 1830

Tyto Ridgway, 1914

Spishi: Angalia katiba
Funga

Mwenendo

Bundi huwinda usiku na hupumzika mchana. Wanamlenga mbuawa wao kwa msaada ya masikio yao. Manyoya ya uso yapeleka mawimbisauti kwa vipenyo vya masikio viliopo mahali tofauti kidogo kimoja kuliko kingine. Hivyo wanaweza kumkamata mbuawa bila kumwona. Mbuawa hawezi kumsikia bundi akija, kwa sababu mabawa ya bundi hayafanyi sauti yo yote kwa kuwa kingo ya mbele ya manyoya ya mabawa imekerezekakerezeka na ile ya nyuma ina matamvua. Hii inapunguza vurugu ya hewa na kwa hivyo uvumi.

Msambao

Familia hii inayosambaa kwenye eneo pana, ingawa haipo katika kaskazini mwa Amerika ya Kaskazini, Sahara ya Afrika na maeneo makubwa ya Asia. Wanaishi katika makazi mengi kutoka jangwa hadi misitu na kutoka kanda za wastani hadi za tropiki. Nyingi za spishi ishirini zilizopo bado za bundi hazijulikani sana. Baadhi, kama bundi mwekundu, wameonekana kwa nadra au kutafitiwa kidogo tu tangu uvumbuzi wao, kinyume na bundi-mabanda ambaye ni mojawapo ya spishi maarufu za bundi duniani. Hata hivyo, nususpishi kadhaa za bundi-mabanda hustahili kuwa spishi tofauti, lakini hazijulikani sana.

Spishi za Afrika

  • Phodilus prigoginei, Bundi wa Kongo (Congo Bay Owl)
  • Tyto alba, Bundi-mabanda (Western Barn Owl)
    • Tyto a. alba, Bundi-mabanda Kaskazi
    • Tyto a. detorta, Bundi wa Kabo Verde
    • Tyto a. hypermetra, Bundi wa Kabo Verde
    • Tyto a. poensis, Bundi Babawatoto au Babewana
    • Tyto a. thomensis, Bundi wa Sao Tome
  • Tyto capensis, Bundi-mbuga (African Grass Owl)
  • Tyto soumagnei, Bundi Mwekundu (Red Owl)

Spishi za mabara mengine


Spishi za kabla ya historia

Picha

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.