Penseli
From Wikipedia, the free encyclopedia
Penseli (kutoka Kiingereza: pencil) ni kifaa cha kuandikia au kuchorea kinachofanywa na kiini thabiti cha grafati au mata nyingine yenye pigmenti kilichopo ndani ya gamba linalokinga kiini kisivunjike.
Penseli inachora kwa kuacha alama za vipande vidogo vya kiini chake kwenye karatasi au uso mwingine unapokandamizwa juu yake.
Penseli ni tofauti na kalamu zinazotoa wino kwenye karatasi.