Kamendegere ni wanyama wakubwa kiasi wa jenasi Pedetes, jenasi pekee wa familia Pedetidae, ambao wanafanana na sungura wenye miguu ya nyuma mirefu au hata na kanguru mdogo, lakini hawana mnasaba na wanyama hawa. Rangi yao ni hudhurungi juu na nyeupe chini. Wanatokea nyika za Afrika ya Kusini na ya Mashariki[1][2]. Hukiakia usiku; wakati wa mchana hupumzika katika matundu yao ambayo wayachimba wenyewe. Hula mimea, mizizi na pengine wadudu. Jike huzaa mwaka mzima, mtoto mmoja kwa mara na mara tatu kwa mwaka.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kamendegere
Thumb
Kamendegere mashariki (Pedetes surdaster)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Rodentia (Wagugunaji)
Nusuoda: Anomaluromorpha (Wanyama kama kindi warukaji)
Familia: Pedetidae (Wanyama walio na mnasaba na kamendegere)
Gray, 1825
Jenasi: Pedetes
Illiger, 1811
Ngazi za chini

Spishi 2:

  • P. capensis (Forster, 1778)
  • P. surdaster (Thomas, 1902)
Funga

Spishi

Spishi ya kabla ya historia

Picha

Marejeo

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.