Panteno
From Wikipedia, the free encyclopedia
Panteno (kwa Kigiriki: Πάνταινος; alifariki 200 hivi[1]) alikuwa mmoja wa wanateolojia wa kwanza katika historia ya Kanisa, mwenye hekima kubwa na ari ya kitume [2].
Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi wa Mashariki na Wakatoliki kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa nao tarehe 22 Juni na 7 Julai[3][4].