Nigeria
From Wikipedia, the free encyclopedia
Nigeria (kwa Kiswahili pia: Nijeria au Naijeria) ni nchi ya Afrika ya Magharibi kwenye pwani ya Bahari Atlantiki.
Ukweli wa haraka
| |||||
Kaulimbiu ya taifa: Unity and Faith, Peace and Progress (Umoja na Imani, Amani na Maendeleo) | |||||
Wimbo wa taifa: Arise O Compatriots, Nigeria's Call Obey (Amkeni wananchi, mtieni wito la Nigeria) | |||||
Mji mkuu | Abuja 9°10′ N 7°10′ E | ||||
Mji mkubwa nchini | Lagos | ||||
Lugha rasmi | Kiingereza | ||||
Serikali Rais Makamu wa Rais |
Shirikisho la Jamhuri Muhammadu Buhari Yemi Osinbajo | ||||
Uhuru kutoka Uingereza |
1 Oktoba 1960 | ||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
923,768 km² (ya 32) 1.4% | ||||
Idadi ya watu - 2015 kadirio - 2006 sensa - Msongamano wa watu |
182,202,000 (ya 7) 140,431,790 188.9/km² (ya 71) | ||||
Fedha | Naira (₦) (NGN ) | ||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
(UTC+1) (UTC+2) | ||||
Intaneti TLD | .ng | ||||
Kodi ya simu | +234
- |
Funga
Imepakana na Benin, Niger, Chad na Kamerun.
Mji mkuu ni Abuja ikitanguliwa na Lagos hadi mwaka 1991.
Nigeria imepata uhuru wake tarehe 1 Oktoba 1960, ikiunganisha maeneo ya koloni la Nigeria na sehemu ya kaskazini ya eneo lindwa la Kamerun ya Kiingereza.
Kwa sasa ni nchi ya Afrika yenye watu wengi na uchumi mkubwa kuliko zote. Kimataifa, ni ya 7 kwa idadi ya watu na ya 20 kwa uchumi.