From Wikipedia, the free encyclopedia
Makala hii inahusu mwanariadha wa Marekani. Kwa makala ya mwandishi wa Puerto Rico, angalia Muna Lee (mwandishi).
Muna Lee (alizaliwa Little Rock, Arkansas, 30 Oktoba 1981) ni mwanariadha wa mbio fupi fupi wa Marekani.
Lee alishinda medali ya dhahabu kama mwanachama wa timu ya Wanawake ya mbio 4 x 100m katika mbio ya Mashindano ya Mabingwa wa Dunia katika Riadha katika mwaka wa 2005. Alikimbia vizuri sana katika mbio za majaribio ya Olimpiki ya 2004,akikimbia kwa kasi katika mkondo wa mwisho na kupita wanariadha wenzake na kushinda nafasi katika timu ya Olimpiki. Aliendelea na akawa nambari 7 katika Michezo ya Olimpiki.
Alishiriki katika michezo ya Olimpiki ya 2008,Beijing akikimbia mbio ya 100m. Katika mbio ya mchujo ya awamu ya kwanza,alikuwa nambari ya kwanza akiwa mbele ya Anita Pisone na Guzel Khubbieva katika muda wa 11.44 s na kuweza kuhitimu awamu ya pili. Katika awamu ya pili ya mchujo aliboresha muda wake ukawa 11.08 na akamaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Sherone Simpson na kuhitimu kukimbia katika nusu fainali. Katika nusu fainali alikimbia na muda wa 11.06s nyuma ya Shelly-Ann Fraser akahitimu kukimbia katika fainali,alichukua nafasi ya tano katika fainali hiyo na muda wa sekunde 11.07 .
Yeye alichukua nafasi ya pili katika Mashindano ya Mabingwa wa Marekani (akiwa nyuma ya Carmelita Jeter) na akahitimu kukimbia katika Mashindano ya Mabingwa katika Riadha wa Dunia wa 2009. Wiki moja kabla ya Mashindano ya Mabingwa wa Dunia ,Lee alikuwa mmoja wa wanawake katika timu ya mbio ya 4 x 100 waliokimbia kwa muda ulio kasi sana katika miaka kumi na miwili. Lauryn Williams, Allyson Felix, Lee na Jeter walimaliza kwa muda wa sekunde 41.58, kuwapa nafasi ya nane kwenye orodha ya muda bora kabisa. [9]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.