Mlangobahari wa Florida
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mlangobahari wa Florida (kwa Kiingereza: Straits of Florida) ni sehemu ya bahari inayotenganisha jimbo la Florida (Marekani) upande wa kaskazini na Kuba upande wa kusini.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/f/f1/Straits_of_florida.png)
Upana wake ni kilomita 150 baina ya visiwa vya Florida Keys na Kuba yenyewe. [1]
Maji yake huunganisha Ghuba ya Meksiko na Atlantiki.
Kati mlangobahari huo unapita mkondo wa Florida unapeleka maji ya vuguvugu kutoka Ghuba ya Meksiko kuelekea kaskazini-mashariki. Maji hayo ni chanzo kikuu cha Mkondo wa Ghuba unaotawala tabianchi za sehemu kubwa za Ulaya.[2]