![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/55/Tanzania_Iringa_location_map.svg/langsw-640px-Tanzania_Iringa_location_map.svg.png&w=640&q=50)
Mkoa wa Iringa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mkoa wa Iringa ni mojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye Postikodi namba 51000. Upo katikati ya nchi, kidogo upande wa kusini. Umepakana na mikoa ya jirani ya Morogoro, Njombe, Mbeya, Singida na Dodoma.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/55/Tanzania_Iringa_location_map.svg/640px-Tanzania_Iringa_location_map.svg.png)
Makao makuu yako katika manisipaa ya Iringa.