![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/0f/Ad%25C4%25B1yaman_districts.png/640px-Ad%25C4%25B1yaman_districts.png&w=640&q=50)
Mkoa wa Adıyaman
From Wikipedia, the free encyclopedia
Adıyaman ni jina la mkoa huko mjini kusini-katikati mwa nchi ya Uturuki. Mkoa huu ulianzishwa mnamo mwaka wa 1954 nje ya sehemu ya Mkoa wa Malatya. Mkoa una eneo la kilomita za mraba zipatazo 7,614. Takriban watu 677,518 (makadirio ya sensa ya mwaka wa 2006, 623,811 (sensa ya 2000)) imezidi kutoka 513,131 kunako mwaka wa 1990. Mji mkuu wa mkoa huu ni Adıyaman. Wakazi waliowengi katika mkoa uu ni Wakurdi.[1]
Ukweli wa haraka Maeneo ya Mkoa wa Adıyaman nchini Uturuki, Maelezo ...
![]() | |
---|---|
Maeneo ya Mkoa wa Adıyaman nchini Uturuki | |
![]() | |
Maelezo | |
Kanda: | Kanda ya Kusinimashariki ya Anatolia |
Eneo: | 7,614 (km²) |
Idadi ya Wakazi | 677,518 TUIK 2007 (est) |
Kodi ya Leseni: | 02 |
Kodi ya eneo: | 0416 |
Tovuti ya Gavana | http://www.adıyaman.gov.tr |
Utabiri wa hali ya hewa | turkeyforecast.com/weather/adıyaman |
Funga
Eneo la mkoani hapa lilikaliwa toka hapo awali na ustarabu kadha wa kadha ulikuwepo hapa. Kuna sehemu kadhaa za kihistoria zinazoweza kuvutia watalii. Nemrud Dağı ni mji mkubwa wenye kuvutia kwa hapa, hasa kwa yale masanamu yaliyojengwa na Antiochus Theos, mfalme wa Commagene.