Milki ya Wasasani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Milki ya Wasasani au Nasaba ya Wasasani (Kiing. Sassanids au Sassanians) ni jina linalotumika kwa nasaba ya Uajemi ya Kale (leo Iran) ambayo ilidumu kutoka 224 hadi 651 BK. [1] [2]
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/9/9b/Sassanid_Empire_620.png)
Milki ya Wasasani ilifuata Waparthi kama watawala wa Uajemi. Ilitambuliwa kwa zaidi ya miaka 400 kama moja ya falme mbili kubwa huko Asia Magharibi, pamoja na Dola la Roma na baadaye Ufalme wa Byzanti.