![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/65/Sprachfamilien_der_Welt_%2528non_Altai%2529.png/640px-Sprachfamilien_der_Welt_%2528non_Altai%2529.png&w=640&q=50)
Lugha za Kihindi-Kiulaya
From Wikipedia, the free encyclopedia
Lugha za Kihindi-Kiulaya ni jamii ya lugha iliyo kubwa kuliko zote duniani. Imekadiriwa kuna lugha hai 445 za jamii hiyo na wasemaji bilioni 3.2 katika mabara yote (46% za watu wote wa leo).
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/65/Sprachfamilien_der_Welt_%28non_Altai%29.png/640px-Sprachfamilien_der_Welt_%28non_Altai%29.png)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/d5/IE5500BP.png/320px-IE5500BP.png)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/c/c8/IE4500BP.png/320px-IE4500BP.png)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/3/36/IE3500BP.png/320px-IE3500BP.png)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/01/IE2500BP.png/320px-IE2500BP.png)
Uenezi huo umetokana hasa na historia ya ukoloni wa Kizungu uliopeleka lugha za Ulaya pande zote za dunia.
Lugha zenye wasemaji zaidi ya milioni 100 ni: Kihispania, Kiingereza, Kihindustani (Kihindi/Kiurdu), Kireno, Kibengali, Kipanjabi na Kirusi.
Nyingine zenye wasemaji zaidi ya milioni 50 ni: Kijerumani, Kifaransa, Kimarathi, Kiitalia na Kiajemi.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/4/4f/IndoEuropeanTree.svg/640px-IndoEuropeanTree.svg.png)