Leodegari wa Autun (kwa Kilatini: Leodegarius; kwa Kifaransa: Léger; Autun, Saône-et-Loire, 615 hivi – Sarcing, Somme, Picardie, 2 Oktoba 679) alikuwa askofu wa Autun, leo nchini Ufaransa, mtoto wa mtakatifu Sigrada [1][2].

Thumb
Kifodini cha Mt. Leger. Mchoro mdogo wa mwaka 1200 hivi unaonyesha alivyotobolewa macho.

Kwa kuwa alimpinga Ebroini, mkuu wa ikulu ya mfalme Theodoriki III, aliyetaka kupindua utawala wa ukoo wa Wamerovinji, aliteswa kikatili, akapofushwa akauawa[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[3]. Pamoja naye anaheshimiwa ndugu yake Warinus aliyeuawa na Ebroini miaka miwili kabla yake kwa kupigwa mawe [4].

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Viungo vya nje

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.