Leodegari wa Autun (kwa Kilatini: Leodegarius; kwa Kifaransa: Léger; Autun, Saône-et-Loire, 615 hivi – Sarcing, Somme, Picardie, 2 Oktoba 679) alikuwa askofu wa Autun, leo nchini Ufaransa, mtoto wa mtakatifu Sigrada [1][2].
Kwa kuwa alimpinga Ebroini, mkuu wa ikulu ya mfalme Theodoriki III, aliyetaka kupindua utawala wa ukoo wa Wamerovinji, aliteswa kikatili, akapofushwa akauawa[1].
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[3]. Pamoja naye anaheshimiwa ndugu yake Warinus aliyeuawa na Ebroini miaka miwili kabla yake kwa kupigwa mawe [4].
Tazama pia
Tanbihi
Vyanzo
Viungo vya nje
Wikiwand in your browser!
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.