![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a2/Basque_Country_Location_Map.svg/langsw-640px-Basque_Country_Location_Map.svg.png&w=640&q=50)
Kieuskara
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kieuskara (au Kibaski) ni lugha hai ya pekee[1] inayotumiwa na Wabaski hasa mpakani mwa Hispania kaskazini na Ufaransa kusini-magharibi kwenye milima ya Pirenei karibu na bahari ya Atlantiki.[2]
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a2/Basque_Country_Location_Map.svg/320px-Basque_Country_Location_Map.svg.png)
Ingawa inakubalika ilikuwa inatumika huko kabla ya lugha za Kihindi-Kiulaya kuenea Ulaya magharibi, haieleweki ilianzaje, kwa sababu hakuna lugha yoyote inayofanana nayo.
Wanaoitumia ni kama watu 715,000, wengi wao wakiwa Hispania, ambako inalindwa na kustawishwa zaidi.