![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a1/Khwarazm.jpg/640px-Khwarazm.jpg&w=640&q=50)
Khorezmia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Khorezmia (pia: Chorasmia) ni eneo la kihistoria upande wa kusini wa Ziwa Aral. Kiini chake ni oasisi kubwa kwenye delta ya mto Amu Darya unapoingia Ziwa Aral. Upande wa mashariki kuna jangwa la Kyzylkum na upande wa magharibi nyanda za juu za Ustyurt. Leo hii eneo limegawiwa kati ya nchi za Uzbekistan, Kazakhstan na Turkmenistan.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a1/Khwarazm.jpg/640px-Khwarazm.jpg)
Wakazi wake walikuwa watu wenye lugha karibu na Kiajemi lakini tangu zama za Kati makabila ya Kituruki yaliingia huko hadi Kiajemi kilipotea.