Enzi ya kati
From Wikipedia, the free encyclopedia
Enzi ya Kati (pia: Zama za Kati; kwa Kiingereza: "Middle Ages", pia "mediaevo" au "medievo") ni kipindi cha katikati cha historia ya Ulaya katika mgawanyo wa “zama” tatu: ustaarabu wa
- Zama za Kale,
- Zama za Kati, na
- Wakati wa Kisasa
ama:
- Enzi ya Kale,
- Enzi ya Kati na
- Enzi ya Kisasa.
Hata kama ugawaji huo umetokana na mazingira ya Ulaya tu, hutumiwa pia kwa maeneo mengine ya dunia. Wataalamu wengi huamini ya kwamba haufai sana kidunia lakini hadi sasa hakuna mpangilio mwingine kwa dunia yote unaoeleweka kirahisi hivi.
Kwa kawaida, Zama za Kati za Ulaya Magharibi huhesabiwa toka mwisho wa Dola la Roma Magharibi (karne ya 5) hadi kuanza kwa falme za kitaifa, mwanzo wa uvumbuzi wa ng’ambo ya Ulaya, kipindi cha mwamko-sanaa, na Matengenezo ya Waprotestanti kuanzia mwaka 1517.
Mabadiliko hayo yalionesha mwanzo wa kipindi cha Zama za Kisasa ambacho kilitangulia mapinduzi ya viwanda.