Jeshi la majini
From Wikipedia, the free encyclopedia
Jeshi la majini au Jeshi la wanamaji ni kitengo cha pekee cha jeshi la mataifa mengi kilicho tayari kushindana na maadui kwenye maji hasa baharini.
Linajumlisha askari, manowari, meli za kuasaidia manowari, mabandari ya pekee na vituo vingine na pia eropleni za vita ya bahari.
Ni hasa nchi zenye pwani la bahari ambako kuna jeshi la pekee la wanamaji. Chanzo katika historia yalikuwa majeshi ya wanamaji ya Karthago, Ugiriki ya Kale na Dola la Roma. Tangu karne ya 19 Uingereza ilikuwa na jeshi la wanamaji kubwa duniani, na katika karne ya 20 nafasi yake ilichukuliwa na wanamaji wa Marekani hasa, lakini pia wa Urusi.
Wikiwand in your browser!
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.