Mahekalu ya Abu Simbel
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mahekalu ya Abu Simbel ni mahekalu mawili makubwa yaliyojengwa zamani za Misri ya Kale. Yanapatikana upande wa magharibi wa Ziwa Nasser katika Nubia, Misri ya Kusini.
Ni maarufu kutokana na uzuri wake na pia kwa sababu yalihamishwa mwaka 1968 kutoka mahali pa awali kando ya mto Nile kwenda mahali pa juu kilimani kwa sababu ya kujaza kwa Ziwa Nasser nyuma ya lambo la Aswan kwa shabaha ya kuyatunza kutoka maji ya ziwa jipya.
Pamoja na mahekalu mengine ya Nubia yameingizwa katika orodha ya urithi wa dunia ya UNESCO.[1]