Haile Mariam Desalegne
From Wikipedia, the free encyclopedia
Haile Mariam Desalegne (* 19 Julai 1965 Boloso Sore, Wolayita, Ethiopia) ni mwanasiasa wa nchini Ethiopia. Mwaka 2010 alikuwa waziri wa mambo ya nje na makamu wa waziri mkuu wa Ethiopia. Baada ya kifo cha waziri mkuu Meles Zenawi terehe 20 Agosti 2012 alikuwa waziri mkuu mtendaji.
Haile Mariam ni kiongozi wa kwanza wa kitaifa anayetoka katika kusini ya Ethiopia na pia mkristo wa kiprotestant wa kwanza katika uongozi wa juu.