Gorée
From Wikipedia, the free encyclopedia
Gorée (kwa Kifaransa: Île de Gorée) ni kisiwa cha Atlantiki mbele ya pwani ya Senegal na sehemu ya manisipaa ya Dakar. Ilijulikana kama kituo cha biashara ya watumwa. Hadi kukomeshwa kwa biashara hiyo mwaka 1848 watumwa walipelekwa kisiwani kutoka bara, kufungwa katika jela, kuuzwa kwenye minada na kusombwa hadi Amerika kwa jahazi.