Dhiraa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Dhiraa (pia ziraa[1], kutoka Kiarabu ذراع dhiraac; ing. ni cubit au ell) ni kipimo cha kihistoria cha urefu cha takriban sentimita 50. Iliitwa pia "mkono".
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/62/Ell.jpg/320px-Ell.jpg)
Ni kati ya vipimo asilia vya Kiswahili, ni umbali mkubwa kati ya kidole kikubwa na kisugudi au kiko cha mkono wake.
Dhiraa inalingana na kipimo cha shibiri; dhiraa moja ni sawa na shibiri mbili.