![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/00/CSIRO_ScienceImage_4350_CSIROs_Parkes_Radio_Telescope_with_moon_in_the_background.jpg/640px-CSIRO_ScienceImage_4350_CSIROs_Parkes_Radio_Telescope_with_moon_in_the_background.jpg&w=640&q=50)
Darubini ya redio
From Wikipedia, the free encyclopedia
Darubini ya redio ni antena maalum na kipokeaji cha redio kinachotumiwa kutambua mawimbi ya redio kutoka kwa vyanzo vya redio kwenye anga-nje. [1] [2] [3] Darubini za redio ndizo vyombo vikuu vya uchunguzi vinavyotumika katika astronomia redio, ambayo huchunguza mawimbi ya redio yanayotolewa na violwa vya anga-nje kama vile nyota, galaksi au nebula. Hivyo zinalingana na darubini nuru zinazochungulia mawimbi ya nuru yanaotoka kwenye violwa vya anga-nje. Tofauti na darubini za nuru, darubini za redio zinaweza kutumika wakati wa mchana na usiku[4].
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/00/CSIRO_ScienceImage_4350_CSIROs_Parkes_Radio_Telescope_with_moon_in_the_background.jpg/640px-CSIRO_ScienceImage_4350_CSIROs_Parkes_Radio_Telescope_with_moon_in_the_background.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/55/UTR-2_-_P3094042_%28wiki%29.jpg/640px-UTR-2_-_P3094042_%28wiki%29.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/63/USA.NM.VeryLargeArray.02.jpg/320px-USA.NM.VeryLargeArray.02.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/6d/FAST_Radio_Telescope_%28captured_from_video%29.jpg/640px-FAST_Radio_Telescope_%28captured_from_video%29.jpg)