Catherine Nakhabi Omanyo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Catherine Nakhabi Omanyo (alizaliwa Kaunti ya Busia, 7 Julai 1978) ni mwanasiasa wa Kenya, mwanaharakati wa elimu, na mwakilishi wa wanawake wa kaunti ya Busia katika Bunge la Kitaifa (Kenya). Anajulikana kwa harakati zake za haki za binadamu, hasa kazi yake ya kutetea haki za wanawake nchini Kenya na kutoa fursa ya elimu kwa watoto maskini na yatima. Anajulikana pia kama mwanzilishi wa Shule ya Kimataifa ya vipaji maalumu, shule isiyo na gharama iliyoko katika Kaunti ya Busia karibu na mpaka na Uganda. [1]