![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/db/Forodhani_jubilee_gardens_Zanzibar.jpg/640px-Forodhani_jubilee_gardens_Zanzibar.jpg&w=640&q=50)
Bustani za Forodhani, Zanzibar
Bustani ya Zanzibar / From Wikipedia, the free encyclopedia
Bustani za Forodhani (pia hujulikana kwa Kiingereza kama Forodhani Gardens, Jubilee Gardens na zaidi hivi karibuni kama Forodhani Park)[1] ni bustani ndogo kwenye Mji Mkongwe wa Zanzibar, Tanzania.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/db/Forodhani_jubilee_gardens_Zanzibar.jpg/640px-Forodhani_jubilee_gardens_Zanzibar.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/17/Zanzibar_2012_06_06_4229_%287592222146%29.jpg/640px-Zanzibar_2012_06_06_4229_%287592222146%29.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/bf/Forodhani_park_food_stand.jpg/640px-Forodhani_park_food_stand.jpg)
Bustani hizo ziko kando ya mtaa wa Mizingani unaopita ukingo wa bahari wa Mji Mkongwe, mbele tu ya majengo ya Jumba la Maajabu (House of Wonders) na Ngome Kongwe (Old Fort). Bustani hiyo ilianzishwa mwaka 1936 na kufunguliwa rasmi tarehe 21 Desemba 1936 kwa maadhimisho ya jubilii ya miaka 25 za utawala wa Sultani Khalifa bin Harub wa Zanzibar (silver jubilee) na pia kwa heshima ya marehemu mfalme George V wa Uingereza aliyewahi kutimiza miaka 25 ya utawala kwenye mwaka 1935[2]. Ilijulikana kama Jubilee Gardens ikabadilshwa jina baada ya mapinduzi ya Zanzibar ya 1964[3].