![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/66/Grass_Owl_adult.jpg/640px-Grass_Owl_adult.jpg&w=640&q=50)
Bundi (Tytonidae)
Ndege mbuai wa familia Tytonidae / From Wikipedia, the free encyclopedia
Bundi (pia mabundi) ni ndege mbuai wa familia Tytonidae na jenasi mbalimbali ya familia Strigidae. Ukurasa huu unahusu familia Tytonidae. Spishi hizi zina rangi ya kahawa nyuma na nyeupe mbele pamoja na madoa madogo meusi. Kichwa chao kina umbo la mviringo na uso mwao una umbo la moyo. Bundi hula ndege na wanyama wadogo, wanyama wagugunaji hasa, lakini wadudu wakubwa pia. Jike huyataga mayai 2-7 kwa mahali palipofunika kama tago lililoachwa na ndege mwingine ndani ya tundu ya mti, ufa wa mwamba, dari la nyumba au kihenge n.k.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...
Bundi | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Bundi-mbuga | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Funga