Vinyama-kigoga (tafsiri la jina la kisayansi) ni wanyama wadogo wa maji matamu na ya chumvi wa faila Bryozoa. Ni wanyama sahili na karibu wote huishi katika makoloni yanayoshikamanisha kwenye nyuso mbalimbali, kama vile miamba, mawe, mchanga, makombe na miani. Kwa kawaida wana urefu wa takriban mm 0.5 na wana muundo maalum wa kujilisha unaoitwa lofofori (lophophore), "taji" ya minyiri inayotumiwa kwa kujilisha kwa njia ya kuchuja. Spishi nyingi za baharini huishi katika maji ya kitropiki, lakini kadhaa hupatikana katika mifereji ya bahari na maji ya maeneo ya ncha za dunia. Vinyama-kigoga wameainishwa kama spishi za baharini (Stenolaemata), spishi za maji tamu (Phylactolaemata) na spishi za baharini na pengine maji ya chumvi kidogo (Gymnolaemata). Spishi hai 5,869 zinajulikana[1]. Spishi za jenasi moja huishi peke yao, nyingine zote huishi katika makoloni.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kinyama-kigoga
Thumb
Koloni ta vinyama-kigoga huko De Beldert, karibu na Tiel, Uholanzi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia
Nusuhimaya: Eumetazoa
Faila ya juu: Lophotrochozoa
Faila: Bryozoa
Ehrenberg, 1831
Ngazi za chini

Ngeli 3, oda 4:

  • Gymnolaemata Allman, 1856
    • Cheilostomata busk, 1852
    • Ctenostomata Busk, 1852
  • Phylactolaemata
    • Plumatellida
  • Stenolaemata Borg, 1926, 1996
    • Cyclostomatida Busk, 1852
Funga

Marejeo

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.