![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/8/8a/OpenMoji-black_1F4F0.svg/langsw-640px-OpenMoji-black_1F4F0.svg.png&w=640&q=50)
Blogu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Blogu ni teknolojia mpya inayowezesha watu binafsi kuchapa maoni na fikra zao katika mtandao wa tarakilishi maarufu kama wavuti au intaneti. Blogu inaweza kuchukuliwa kama ni shajara pepe.
![Uandishi wa Blogu](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/8/8a/OpenMoji-black_1F4F0.svg/320px-OpenMoji-black_1F4F0.svg.png)
Neno la Kiswahili "blogu" linatokana na neno la Kiingereza, "blog", ambalo limetokana na neno lingine, "weblog".
Kimsingi, blogu ni aina ya tovuti ambayo huandikwa mara kwa mara na kwa mpangilio wa mambo mapya kutokea ukurasa wa mbele kuendana na tarehe na mwezi.