Beatriz wa Silva
From Wikipedia, the free encyclopedia
Beatriz wa Silva, O.I.C. (jina kamili kwa Kireno: Beatriz de Menezes da Silva; Campo Maior, Ureno[1] 1424 hivi – Toledo Hispania, 9 Agosti 1492) alikuwa mwanamke wa ukoo maarufu wa Ureno, lakini alijiunga na monasteri na hatimaye akawa mwanzilishi wa masista wamonaki wa Shirika la Bikira Maria Kukingiwa Dhambi ya Asili.
Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu bikira.