![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/ac/Irish_Sea_%25E2%2580%2593_relief%252C_ports%252C_limits.tif/lossy-page1-640px-Irish_Sea_%25E2%2580%2593_relief%252C_ports%252C_limits.tif.jpg&w=640&q=50)
Bahari ya Eire
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bahari ya Eire (kwa Kiingereza: Irish Sea) ni sehemu ya bahari inayotenganisha visiwa vya Eire (Ireland) na Britania.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/ac/Irish_Sea_%E2%80%93_relief%2C_ports%2C_limits.tif/lossy-page1-640px-Irish_Sea_%E2%80%93_relief%2C_ports%2C_limits.tif.jpg)
Ndani yake kuna visiwa viwili vikubwa kiasi ambayo ni Anglesey (Welisi) na Isle of Man, pamoja na visiwa vidogo.
Inapakana na nchi za Welisi, Uingereza na Uskoti (zote sehemu za Ufalme wa Muungano) upande wa mashariki, halafu Eire na Eire ya Kaskazini (pia sehemu ya Ufalme wa Muungano) upande wa magharibi.
Kila mwaka kuna abiria milioni 12 wanaovuka bahari hii na bidhaa tani milioni 17 zinasafirishwa kati ya Britania na Eire.