Apostolicam Actuositatem
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mtaguso wa pili wa Vatikano uliwaongelea walei katika hati mbalimbali ukionyesha nafasi yao katika maisha ya Kanisa (liturujia, upashanaji habari, ekumeni n.k.).
Hata hivyo uliona umuhimu wa kuwaandikia hati maalumu iwaongoze hasa katika utume ili watimize wajibu wao kwa wokovu wa ulimwengu.
Karibu waamini wote wa Yesu ni walei, tena ndio wanaoshirikiana zaidi na watu wowote katika yote: hivyo wasipotoa mchango wao, utume wa Kanisa utakuwa mlemavu, hasa siku hizi.
Si kwamba wanapaswa kufanya utume kutokana na uhaba wa mapadri na watawa, bali kutokana na wito walioupata katika ubatizo na kipaimara.
Hati hiyo, ilitolewa tarehe 18 Novemba 1965 kwa kura 2340 dhidi ya 2 tu, inaanza na maneno "Apostolicam Actuositatem" (katika Kilatini yana maana ya "Utendaji wa Kitume").