![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e5/Atlantic_Coast_%25282308232123%2529.jpg/640px-Atlantic_Coast_%25282308232123%2529.jpg&w=640&q=50)
Alasiri
From Wikipedia, the free encyclopedia
Alasiri (kutoka Kiarabu) ni kipindi cha mchana kati ya adhuhuri na jioni, wakati ukali wa mwanga wa jua unapozidi kupungua.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e5/Atlantic_Coast_%282308232123%29.jpg/640px-Atlantic_Coast_%282308232123%29.jpg)
Kwa kawaida wakati huo kwa binadamu unafuata mlo: hivyo utendaji wake unapungua pamoja na umakinifu wake. Ndiyo sababu ajali nyingi huwa zinatokea wakati huo.
Dini mbalimbali zenye ratiba ya sala, kwa mfano Ukristo na Uislamu, zina kipindi maalumu kwa alasiri.